Download Mp3 from African

Mwanamitindo agongwa na treni akipigwa picha Marekani

Mwanamke wa umri wa miaka 19, ambaye alikuwa anaanza kujikuza kama mwanamitindo, aligongwa na treni na kufariki alipokuwa anapigwa picha.

Fredzania Thompson alikuwa anapigwa picha hizo zake za mitindo, ambazo zilikuwa za kwanza, kwenye reli alipogongwa na gari moshi.
Picha za Thompson, alizopigwa muda mfupi kabla ya mkasa huo kutokea Navasota, Texas, zimesambazwa na familia yake.
Polisi wanasema alikuwa mjamzito wakati huo na kwamba alikuwa anaondokea treni moja kwenye njia moja ya reli alipojipata ameingia kwenye njia ya reli ambapo kulikuwa na treni nyingine iliyokuwa inapita ambayo ilimgonga.
Gazeti la The Eagle limesema ilikuwa mara yake ya kwanza kwenda kupigwa picha za uanamitindo.
"Bila shaka, hilo jambo alililotaka kulifanya maishani," Hakamie Stevenson alisema kumhusu bintiye.
"Ndiyo shughuli aliyoanza kuifanya siku aliyokumbana na mauti yake."
Polisi wanasema bado wanafanya uchunguzi kuhusu kisa hicho.
Ukurasa umefunguliwa katika mtandao wa GoFundMe kujaribu kuchangisha $10,000 (£8,150) za kugharimia mazishi ya Fredzania.


Tag : EXCLUSIVES, News
Back To Top