Mabalozi wa usalama barabarani mkoani Arusha wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kushiriki katika wiki ya nenda kwa usalama iliyozinduliwa hivi karibuni mkoani hapo.Picha na Vero Ignatus Blog.
Balozi Vero Ignatus akisalimiana na mkuu wa wilaya mkuu wa wilaya ya Arusha Mjini Gabriel Daqqaro ambaye alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Arusha alipowasili katika uwanja wa Shekh Amri Abeid na kupokelewa na kamati ya maandalizi ya mkoa ya usalama barabarani.Picha na Vero Ignatus Blog.
Na Vero Ignatus Arusha.
Operesheni abiria paza sauti inatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni katika mkoani Arusha ikiwa na lengo la kumuelimisha abiria pamoja wanawatumiaji wa vyombo vya moto kuwa makini kutii na kufuata sheria za usalama barabarani .
Hayo yamesema na mwenyekiti wa mabalozi wa usalama barabarani Stella Rutaguza alipokuwa kwenye wiki ya nenda kwa usalama iliyozinduliwa hivi karibuni mkoni Arusha amabapo kilele chake kilikuwa tar 11novemba katika uwanja wa mpira Shekh Amri Abed jijini Arusha.
Stella amesema kuwa abiria anatakiwa kufunga mkanda akiwa ndani ya chombo cha usafiri,kuripoti vitendo vyote vinavyohatarisha usalama wa abiriaikiwemo mwendo kasi,ulevi wa dereva,upitaji wa hatari wa magari mengine bila kufuata sheria na alama za barabarani,dereva kuzun gumza na simu akiwa anaendesha,pamoja na lugha chafu ya uhasama kwa abiria.
Bi Rutaguza amesema kuwa jukumu la kuzifanya barabara zetu kuwa salama ni la kila mtu ,hivyo kila mmoja anatakiwa kutimiza wajibu wake,tusiwaachie askari wa usalama barabarani peke yao kwani hawawezi kuwa kila mahali.
“Suala la usalama barabarani ni la kila mtu ,maana usipotumia usafiri binafsi utatumia usafiri wa jumuia,au hata pikipiki ilimradi umesafiri ndiyo maana kila mmoja anatakiwa awe mlinzi wa mwenzie ,kwa kutoa taarifa pale unapoona dereva anakiuka sheria ya usalama barabarani ili tuweze kuepuka ajali zinazosababishwa na uzembe pamoja na ulemavu”alisisitiza Bi Stella.
Amesema kuwa operesheni paza sauti inafanyika kwa miezi mitatu ikiwa na lengo la kuelimisha ,kukemea,na kutoa ripoti kwa jeshi la polisi kitengo cha isalama barabarani,abiria kufahamu haki yake awapo ndani ya chombo cha usafiri,hatakiwi kukaa kimya aonapo dereva anavunja sheria za usalama barabarani.
Ameainisha haki za abiria kwa mujibu wa kanuni za usafirishaji za Sumatra,abiria kurudishiwa nauli chombo kinapochelewa kuanza safari ndani ya saa mbili au chombo kuharibika,kupewa tiketi ndani ya ofisi,kutonyanyaswa kwa lugha ya matusi,abiria kufikishwa mwisho wa safari,kulipa nauli iliyoidhinishwa na Sumatra na nyingine nyingi.
Amewataka abiria wasikubali kuchanganywa kwenye vyombo vya usafiri pamoja na wanyama,au mizigo ya hatari ndani ya gari kama vile misumari,gesi, na milipuko, amesema abiria anatakiwa afahamu kuwa yeye siyo mateka wa dereva bali ana haki ya kusafiri salama kutokana na nauli aliyolipa,ambayo ni mkataba kati yake na mwenye gari na siyo upendeleo.
Tag :
lainnya