Download Mp3 from African

SENSEI KALONGA:KARATE NI TAALUMA NDIYO MAANA KUNAMAFUNZO KILA MWAKA



Tamasha hilo limeandaliwa na chama cha karate mkoa wa Kilimanjaro huku ambapo zaidi ya vijana 54 wa kike v na wakiume 49 walishiriki katika mchezo huo,ambapo umeshirikisha vilabu viwili tofauti  ambavyo ni Mo town lodge na Suparampe zote zinatoka manispaa ya Moshi mjini.

Raisi wa Shirikisho la karate nchini Tanzania na mwenyekiti wa chama cha karate mkoani Kilimanjaro Sensei Kalonga amesema kuwa vijana hao wamepata mafunzo kwa  mwaka mmoja na niutaratibu wa chama cha karate.

Kalonga amesema kuwa wameandika historia mpya kwa kuupigania mchezo wa karate mkoa wa kilimanjaro na Tanzania nzima,pia  umuhimu wa maendeleo ya vijana kupitia mchezo wa Karate,amesema mchezo huo ni taaluma ndiyo maana wamekaa darasani na kufuzu.

"tumieni mafunzo mliyoyapata vizuri mahali popote mtakapokuwepo zingatieni nidhamu ,upendo pamoja na maadili yote mliyofundishwa huku mkiwa mfano bora wa kuigwa katika jamii,nyie ndio mkataokuwa barua ya kusomeka kwa jamii kuwa karate siyo mchezo wa kihuni

Makamu mwenyekiti wa cha Karate mkoani Kilimanjaro Sensei Hamza Mzonge amesema kuwa karate siyo mchezo wa kihuni kama baadhi ya watu wadhaniavyo,bali msingi mkuu wa Karate ni Nidhamu ,moyo safi,na kuiheshimu jamii kwa ujumla pamoja na familia kwa ujumla.

Sensei Hamza amesema kuwa karate inatengeneza afya ,kudumisha nidhamu,karate haitumiki kuvunja nidhamu ,bali ni mchezo kama michezo mingine na unakanuni zake ,ni tofauti na vile ambavyo watu wandhania lazima uheshimiwe na kila mwanakarate.

"Tunaposema karate haina kufuzu ni kweli ,maana mie mwenyewen ni mkufunzi lakini hadi leo bado naendelea kujifunza siku zote,tudumishe nidhamu,mtu yeyote yule anayevunja nidhamu katika karate siyo katateka alisisitiuza sensei Hamza.

Kwa upande wake sensei Ibrahim Mganga amewataka wahitimu hao kuwa mfano bora haswa katika kuwa na moyo safi huku alisisiktiza kuwa karate ni nidhamu na moyo safi ndiyo sababu huwa wanavaa mavazi meupe kama ishara ya usafi.

"tunavaa mavazi meupe hili vazi linaonyesha usafi na mara zote ukivaa nguo nyeupe utajilinda ili usilitie doa maana litaonekana na kuweka dosari,hivyo basi karate ni zaidi ya vazi jeupe msitumie karate vibaya ikaja ikaonekana ni ya ovyo ndiyo sababu karate siku zote msingi wake ni NIDHAMU"alisisitiza sensei Ibrahim
 
Aliyepo katikati ni rais waShirikisho la Karate nchini Tanzania ambaye pia ni mkufunzi wa Gojuliu Karate Mkoa wa Kilimanjaro Sensei Geofrey Kalonga,wakwanza kulia ni Sensei Hamis Wembo ambaye ni mkufunzi wa polisi mkoa wa Kilimanjaro ambaye pia ni Katibu mkuu wa Chama cha Karate mkoa wa Kilimanjaro,aliyepo kulia kwake ni Mkufunzi wa chuo cha polisi Moshi( CCP)Sensei Ibrahim Mganga ,wakiwa katika tamasha la kuwatunuku vyeti wanafunzi wa katare waliofuzu mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa shule ya msingi Mwenge iliyopo Manispaa ya Moshi Mjini.Picha na Vero Ignatus Blog.
Club mbili za Karate wakiwa katika maonyesho ya pamoja katika tamasha lilifanyika katika shule ya msingi mwenge iliyopo Manispaa ya Moshi mjini,ambazo ni Mo town Club na suparampe lodge zpte za Moshi  mjini.Picha na Vero Ignatus Blog.

Mwanadada Matilda Mallya akifanya yake katika karate kwenye tamasha hilo la kukabidhiwa vyeti kwa wahitimu lililofanyika katika ukumbi wa Shule ya Msingi Mwenge iliyopo Manispaa ya Moshi mjini ambapo yeye alipewa cheti kwa kufuzu mafunzo ya mkanda wa brown.Picha na Vero Ignatus Blog.




Tag : lainnya
Back To Top