Download Mp3 from African

Omario Lee na Love-B Yuda kumkubali B Face kuwa ye ndiye mwana hip hop Bora


Omario Lee, B Face & Love B Yuda
Si jambo raisi msanii kumkubali msani mwingine kama wanavyo mkubali B Face, mwana hip hop Omario Lee mkali wa "Hema Water" mwenye makazi yake nchini Uganda, amemumwagia sifa nyingi mwana hip hop B Face mkali wa "Sisomeki".

Omario lee amesema kuwa baada ya kuingia  kwenye game ya muziki, kwa mtazamo wake wakaribu amegundua mwana hip hop B Face ni mkali zaidi nchini Burundi, na kazi zake zinakubalika kwasababu anapenda kubuni kwa namna anavyo jiendeleza kwenye game ya muziki ya Republic of Burundi Fleva.

Aidha, mwana hip hop mwingine ajulikanae kwajina la Love-B Yuda mwenye makazi yake pia nchini Uganda, amemsifia sana na kusema kuwa B Face ndiye mwana hip hop mahiri nchini Republic of Burundi huku akisisitiza nakusema kuwa B Face ni msani wa kuiga,

"kile ambacho namkubali zaidi  B Face, anavyo jiendeleza kwenye game hii na pia anaitangaza vizuri  Hip Hop, anaupendo mkubwa kwa wasqni wengine pia wengi wanazidi kuiga kupitia kwake endapo ataendelea ivo atqifikisha mbali muziki wa Hip hop katika tuzo kubwa kubwa za afrika ata duniani, kwa upande wangu ni mkali zaidi, big upwards B Face", amemalizia Yuda.
Back To Top