Download Mp3 from African

KWAKUTOKUZINGATIA VIGEZO KWA KWAMISHA RUFAA YA LEMA




Wafuasi wa chadema wakiwa wamevalia tshirt zilizoandikwa Justice iv Lema mahakamani jana.Picha na Vero Ignatus Blog.
Watu wakiwa nje ya maakama jana .Picha na Vero Ignatus Blog






Na .Vero Ignatus Arusha.
Wafuasi
Upande wa jamhuri waweka pingamizi juu ya rufaa  hiyo iliyokatwa ya kusikiliza pingamizi ya uamuzi wa mahakama ya hakimu mkazi juu ya kumnyima dhamana mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema.

Akizungumza na waandishi wa habari ,Wakili mwandamizi  Mahakama kuu ya kanda ya Arusha ,Matenus Marando ,alisema wameweka pingamizi la rufaa hiyo kutokana na upande wa utetezi kushindwa kuzingatia vigezo vya ukatwaji wa rufaa hiyo 

Alisema kuwa vigezo hivyo  kwa  upande wa utetezi hawakuonesha nia ya kukata rufaa kwa kuandika notisi ya rufaa na badala yake walikata rufaa bila kufuata utaratibu huo .

Wakili Marando alisema kuwa  kulingana na kifungu cha sheria cha 361(1)(a) cha CPA kilimtaka mkataji rufaa kuonesha nia ya kukata rufaa kwa kuandika notisi ya rufaa  na si kukata hivyo waliitaka mahakama itupilie mbali rufaa hiyo 

""Tulikuja na pingamizi na tukawapatia upande wa pili baada ya hapo tulienda kwa jaji Fatuma Massengi ,tumekubaliana kuwa hilo pingamizi lisikilizwe kwanjia ya maandishi ,"alisema Marando  

"Hivyo tarehe xxx tutawasilisha pingamizi letu saa ii asubuhi ,saa vi mchana upande wa utetezi utajibu ,saa 10 upande wa serikali utajibu hoja lakini tarehe ii uamuzi utatolewa na mahakama juu ya pingamizi letu ,"alisema Marando 

"Kama pingamizi letu likishindwa basi rufaa itasikilizwa na kama litashinda basi watatakiwa tena kukata rufaa kama sheria ilivyoangiza,


Upande wa wakili wa utetezi ,Peter Kibatala ,alisema kikubwa kitakachoenda kubishaniwa ni muda uliotumika kuleta hitaji ya kusudi la kukata rufaa  ambako itaenda kuangaliwa kama ilikuwa lipo ndani ya muda au nje ya muda.
Tag : lainnya
Back To Top