SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limeburuzwa mahakamani na wakazi 87 waliokopeshwa nyumba za mradi wa shirika zilizoko Kijichi jijini Dar es Salaam, wakiiomba lisiwabugudhi hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa.
Kesi hiyo imefunguliwa na wakazi hao katika Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, wakilalamikia Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF na Kampuni ya Majembe Auction Mart. Kesi hiyo ilipangwa kutajwa jana mbele ya Jaji Penterine Kente.
Wakili wa walalamikaji hao, Benito Mandele, amewasilisha maombi mahakamani hapo kutaka itoa amri ya kutokubugudhiwa na mazingira ya makazi hayo yabaki kama yalivyo hadi kesi yao ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.
Katika kesi ya msingi, mbali na NSSF, mlalamikiwa wa pili ni Majembe ambaye hakufika mahakamani. Wakili Mandele alidai kuwa alipeleka wito wa mahakama katika ofisi yake iliyoko Mwenge, lakini hakufanikiwa kumpata kwa kuwa amehamisha ofisi eneo hilo.
Tag :
lainnya