Download Mp3 from African

Tukio la kushangaza mwili wa Albino wafukuliwa kabulini ili kufanyiwa uchunguzi uko mkoani Shinyanga

Mwili wa   Michael Juma  mwenye umri wa miaka  miwili na nusu  ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino) kaburi lake lililazimika  kufukuliwa kwa ulinzi wa jeshi la polisi  ili  mwili ufanyiwe uchunguzi kutokana na kuibuka  maneno  yenye kutatanisha  wakati alipokuwa akiugua alivuja damu nyingi  puani na kuvimba mwili.
 
Tukio  la kufukua kaburi hilo  ambalo mwili wa marehemu  mtoto  huyo  alikuwa amezikwa tangu siku ya Jumapili  pembeni ya nyumba waliyokuwa wakiishi na wazazi wake   limetokea juzi  siku ya alhamisi  katika kijiji cha Bunambiyu halmashauri ya wilaya ya Kishapu  mkoani Shinyanga nakuwashangaza wakazi wa eneo hilo.

 
Katibu wa chama cha  albino  (Tas) mkoani Shinyanga Lazaro Anael  alisema kuwa kitendo cha kuufukua mwili  kimewashangaza  tangu alipopata taarifa kuwa kifo cha mtoto huyo  kumezuka maneno kuwa kina utata wakati yeye alishiriki mazishi

Naye diwani wa kata ya Bunambiyu  Richard Sangisangi  aliyekuwa amekataa mwili huo kufukuliwa nakugoma kuwaita majirani kwaajili ya kufukua mwili.
 
 Mwenyekiti wa kijiji hicho  Jonathani  Katela  alisema kuwa kitendo cha kufukua mwili hali hiyo itarudisha tena majonzi kwa jamii na familia  lakini kama serikali imeamua kufanya hivyo basi.
 
Tag : lainnya
Back To Top