Download Mp3 from African

PICHA : Inter Star Kuitambia Messagé Ngozi, LLB kufanya vizuri dakika za mwisho na Flambeau imeonesha ubabe wake

Timu ya AS Inter Star imeitambia  Messagé Ngozi kwa mabao 2-1 dhidi ya Messagé Ngozi , jana Jumamossi kwenye Uwanja wa Mwana Mfalme Prince Louis Rwagasore.
 Mechi imekuwa ya kupendeza sana huku timu ya kutoka mkoani Ngozi imeonekana ikimiliki mpira sana kama kawaida ya timu hiyo ila mwishowe wamepatwa na mshangaho kuona mechi imemalizika kwa ushindi wa timu ya mjini Bujumbura Inter Star kupitia mchezaji  kongwe wa timu hiyo ajulikanaye kwajina la Puchu de Guerre ambae ameingia kipindi chapili na kuleta mabadiliko makubwa huku akifanikiwa kuona lango dakika ya mwisho kwa kuizawadia timu yake ushindi. 

Tuwakumbushe kuwa  Messagé Ngozi ina pointi tatu tu katika mechi tatu baada ya kuifunga Vitalo bao 1-0 katika mechi ya kwanza huku mechi mbili imepoteza kwa matokeo isiyo ridhisha ya tatu bila ikiwa nyumbani kwake Ngozi dhidi ya Atletico Olympic pia na jana 2-1 dhidi ya Inter Star.

 kwasasa timu ya As Inter star inazidi  kuongoza  baada ya kufanya vizuri mechi tatu ikiwa na pointi zote tisa na kuwa kileleni sambamba na  LLb Academic. 
Katika wiki ya tatu ya Ligi Kuu Primus League, LLb imepata ushindi wake kwa shiai wa bao 1-0 dhidi ya Muzinga, Flambeau De l'Est ya Ruyigi imefanya vizuri ugenini na kupata ushindi wa bao 1-0  dhidi ya Buja City kupitia mchezaji wake nyota ajulikanae kwajina la Dubien pia Les Lierres imeridhika kwenda sare ya 1-1 dhidi ya Messagé  Bujumbura. Mechi zingine zitaendelea leo na  matokeo bila shaka mtazipa hapa.

Picha chache za Inter Star 2-1  Messagé Ngozi

Back To Top